Chapter 1.1 (Kiswahili 5)

Kusikiliza na kuzungumza

Matamshi bora – Silabi na vitanzandimi

sauti f na v, s na z, l na r, na th na dh

Shughuli 1: Kutambua silabi

1. Tazameni picha hizi mkiwa wawiliwawili. Mweleze mwenzako umeona nini.

fu

vi

sa

zi

li

ro

dha

the

2.

(a) Tamka maneno yafuatayo ukiwa na mwenzako:

figa

vuna

ugali

sahani

thelathini

kiazi

samaki

tangawizi

karoti

jokofu

maharagwe

pilipili

dhuru

(b) Mwonyeshe mwenzako silabi za sauti f na v, s na z, l na r, th na dh katika maneno uliyotamka.

Shughuli 2: Kutamka silabi

1. Ukiwa na mwenzako, tamkeni silabi zifuatazo kwa zamu:

(a) Silabi za sauti f na v

fa, fe, fi, fo, fu

va, ve, vi, vo, vu

(c) Silabi za sauti l na r

la, le, li, lo, lu

ra, re, ri, ro, ru

(b) Silabi za sauti s na z

sa, se, si, so, su

za, ze, zi, zo, zu

(d) Silabi za sauti th na dh

tha, the, thi, tho, thu

dha, dhe, dhi, dho, dhu

2. Elekezwa na mwalimu au mwenzako kutamka silabi zile zinazokutatiza.

Shughuli 3: Kutamka vitanzandimi

Ukiwa na mwenzako, tamkeni vitanzandimi vifuatavyo kwa zamu:

  1. Fatiha alivua na kufua vazi alilovaa.
  2. Mvuvi mvivu alishindwa kufunga nyavu za kuvua.
  3. Kasa wa ziwani amejikaza kisabuni.
  4. Mzee wa sita alisita kusoma saa zote.
  5. Shirika la reli larejelea shughuli zake rasmi.
  6. Hili ni trela na lori la Lolwe.
  7. Dhamira thabiti ni dira dhahiri maishani.
  8. Kidhibitimwendo madhubuti ni cha thamani.

Shughuli 4: Kuunda vitanzandimi

Shirikiana na mwenzako kuunda vitanzandimi ukitumia maneno haya:

(a) vua/fua

(c) kura/kula

(b) sisi/zizi

(d) thamani/dhamani

Changamka

Tumia kifaa cha kidijitali kama vile simu kujirekodi ukitamka vitanzandimi kisha usikilize utamkaji wako. Mpe mlezi wako pia asikilize matamshi yako.

Chora mchoro huu daftarini kisha ujitathmini.

ndiyo

Ninaweza kwa kiasi kidogo.

Ninahitaji kufanya mazoezi zaidi.

Ninaweza kutamka vitanzandimi.

Please wait