sauti f na v, s na z, l na r, na th na dh
Shughuli 1: Kutambua silabi
1. Tazameni picha hizi mkiwa wawiliwawili. Mweleze mwenzako umeona nini.
fu
![](https://opiqke.blob.core.windows.net/kitcontent/7538b398-35f8-49e6-b688-1261dfea3b3c/10de90ef-ed9b-49fd-b671-65d39ca9485c/9a21c009-0858-486b-b2d9-1494c6b07b94_m.jpg)
vi
![](https://opiqke.blob.core.windows.net/kitcontent/7538b398-35f8-49e6-b688-1261dfea3b3c/d32a44fd-18ed-4f80-b096-e5ff37ed87cb/9cb6d43f-3daa-407c-ba59-f0d30478ebe8_m.jpg)
sa
![](https://opiqke.blob.core.windows.net/kitcontent/7538b398-35f8-49e6-b688-1261dfea3b3c/13b78f68-d0dd-449a-9c97-50cce123c46e/a841970b-c728-40a7-a76d-225b20da0eba_m.jpg)
zi
![](https://opiqke.blob.core.windows.net/kitcontent/7538b398-35f8-49e6-b688-1261dfea3b3c/b074996c-0a79-4af3-9bde-44bbbe5a56fe/bc9d7a3b-0bb5-45af-b7db-d7702c33c3f4_m.jpg)
li
![](https://opiqke.blob.core.windows.net/kitcontent/7538b398-35f8-49e6-b688-1261dfea3b3c/692f4a7c-807a-4a96-b477-9b99114a1f27/a0d38fe5-5ab4-4771-999c-b81c7804ac1c_m.jpg)
ro
![](https://opiqke.blob.core.windows.net/kitcontent/7538b398-35f8-49e6-b688-1261dfea3b3c/ac4834b9-cc12-4e2d-8c32-e2e0b11a4148/ccafbb18-dff5-40d4-ba07-89aa330bdc95_m.jpg)
dha
![](https://opiqke.blob.core.windows.net/kitcontent/7538b398-35f8-49e6-b688-1261dfea3b3c/cade6430-6ba2-44b6-8bf7-99aaec1cd7d9/3f899687-fd1b-4039-bb3b-1ec3714e6e95_m.jpg)
the
![](https://opiqke.blob.core.windows.net/kitcontent/7538b398-35f8-49e6-b688-1261dfea3b3c/8067133b-fd52-4f05-8d9d-74ffbb624a4f/85cacbcd-558f-402d-88ec-1f9df29fb99e_m.jpg)
2.
(a) Tamka maneno yafuatayo ukiwa na mwenzako:
figa vuna ugali sahani thelathini | kiazi samaki tangawizi karoti | jokofu maharagwe pilipili dhuru |
(b) Mwonyeshe mwenzako silabi za sauti f na v, s na z, l na r, th na dh katika maneno uliyotamka.
Shughuli 2: Kutamka silabi
1. Ukiwa na mwenzako, tamkeni silabi zifuatazo kwa zamu:
(a) Silabi za sauti f na v fa, fe, fi, fo, fu va, ve, vi, vo, vu | (c) Silabi za sauti l na r la, le, li, lo, lu ra, re, ri, ro, ru |
(b) Silabi za sauti s na z sa, se, si, so, su za, ze, zi, zo, zu | (d) Silabi za sauti th na dh tha, the, thi, tho, thu dha, dhe, dhi, dho, dhu |
2. Elekezwa na mwalimu au mwenzako kutamka silabi zile zinazokutatiza.
Shughuli 3: Kutamka vitanzandimi
Ukiwa na mwenzako, tamkeni vitanzandimi vifuatavyo kwa zamu:
- Fatiha alivua na kufua vazi alilovaa.
- Mvuvi mvivu alishindwa kufunga nyavu za kuvua.
- Kasa wa ziwani amejikaza kisabuni.
- Mzee wa sita alisita kusoma saa zote.
- Shirika la reli larejelea shughuli zake rasmi.
- Hili ni trela na lori la Lolwe.
- Dhamira thabiti ni dira dhahiri maishani.
- Kidhibitimwendo madhubuti ni cha thamani.
Shughuli 4: Kuunda vitanzandimi
Shirikiana na mwenzako kuunda vitanzandimi ukitumia maneno haya:
(a) vua/fua | (c) kura/kula |
(b) sisi/zizi | (d) thamani/dhamani |
Changamka
Tumia kifaa cha kidijitali kama vile simu kujirekodi ukitamka vitanzandimi kisha usikilize utamkaji wako. Mpe mlezi wako pia asikilize matamshi yako.
Chora mchoro huu daftarini kisha ujitathmini.
ndiyo | Ninaweza kwa kiasi kidogo. | Ninahitaji kufanya mazoezi zaidi. | |
Ninaweza kutamka vitanzandimi. |